Ushindi Kwenye Mtihani Wa Ufahamu Wa Biblia

Pongezi wa Umoja wa Vijana Usharika wa Kiluvya kwa kuwa washindi katika mitihani yao ya Ufahamu wa biblia katika ngazi ya Jimbo na Dayosis

Picha: Baadhi ya Vijana wakifurahia Ushindi wao, Katika Ngazi ya Jimbo na Dayosisi.

Picha :Baadhi ya vijana walioshiriki katika Mitihani ya Ufahamu wa Biblia ngazi ya Jimbo na Dayosisi

Picha:Vijana wakiwa na Mwenyekiti wa Vijana Ngazi ya Dayosisi Bw Anania J Ndondole mwenye tai, Na Mwenyekiti wa Vijana Usharika wa Kiluvvya aliyevaa koti la dark blue Bw Haleluya Ngao

Picha Mkuu wa Jimbo la Magharibi Rev J Mwangomola akifurahi Ushindi wa Vijana KKKT Kiluvya 
Picha: Vijana KKKT Kiluvya walipokuwa wakikabidhi kikombe cha Ushindi wa mtihani wa Biblia walichoshinda Ngazi ya Jimbo katika Usharika wetu.



0 comments:

Yote Huanza Na Mungu




Nawasalimu katika Jina la Yesu, Bwana na mwokozi wa maisha yetu, Neema ya Mungu na Upendo wake Uwe nanyi daima,


Kuelekea katika Tamasha la Vijana, KKKT-DMP Usharika wa Kiluvya, ambalo linatarajia kufanyika tarehe 28/4/2017 lenye ujumbe mkuu " Find Your Purpose " likimaanisha tafuta KUSUDI la maisha yako, Umoja wa vijana kiluvya unapenda kuwaalika walengwa wote wa tamasha hilo kuhudhuria bila kukosa. 

Mara nyingi hili swali la kujua kusudi ya maisha yako huwa linawatatiza wengi, na vitabu vingi vimeandika kwa ajili ya kutoa majibu ya hili swali, "nini kusudi la maisha yangu?". Na mara nyingi tunajiuliza maswali mengi kibinafsi kama Je nataka kuwa nani, nifanye nini na maisha yangu? Malengo yangu ni Yapi?

 "Kwa kua katika yeye vitu vyote viliumbwa vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, Vinavyoonekana na visivyoonekana, ikiwa ni vitu vya enzi au usultani au enzi, au mamlaka;vitu vyote viliumbwa kwa  njia yake, na KWA AJILI YAKE"(Wakolosai 1:16) Hivyo basi kusudi lako katika maisha linaanza na Mungu.

Napenda kuwakaribisha katika Mkesha huu Mkubwa wa kumsifu na kumwabudu Mungu, kwa kutambua kwamba tumeumbwa kwa ajili yake na kusudi la maisha yetu linaanza na Yeye.

Yote Huanza na Mungu

0 comments:

Utangulizi

Post hii imetambulishwa kama utangulizi kutokana na video  na link zilizowekwa ambazo zote zinakupa nyimbo zilizoimbwa na kwaya ya vijana KKKT kiluvya. Wengi wa vijana hao  wapo pia katika Umoja wa Vijana wa Usharika wa Kiluvya.

Post hii, itakupa fursa ya kuwafahamu kwa sura wengi wa vijana hao wanaojitoa kwa ajili ya kanisa kwenye shughuli mbalimbali hasa Uinjilisti kwa njia ya Uimbaji.

Kwaya Ya Vijana KKKT Kiluvya 
Wimbo: Mahangaiko




Bonyeza hii link kwa ajili ya kuuona wimbo wa "Tumia Vyema Uwezo wako" wa kwaya ya vijana KKKT kiluvya https://www.youtube.com/watch?v=JbsAiS2R28E


Asanteni kwa kutubariki na ujumbe wenu katika hizi nyimbo kwamba Mahangaiko yetu yesitupeleke mbali na Neema ya Mungu, na vile vile tutumie vyema uwezo (kipaji/Nafasi) wetu.

Katika kutumia vipawa walivyokirimiwa na Mungu, Umoja wa vijana KKKT-DMP Usharika wa Kiluvya umeanda   Tamasha la Mkesha wa Kuabudu na Kusifu litakalofanyika siku ya Ijumaa tarehe 28/04/2017 kuanzia saa tatu kamili Usiku.


4 comments:

Copyright © 2017 Umoja wa Vijana KKKT Kiluvya